Departments

Idara ya Maendeleo ya Utamaduni

MAJUKUMU YA IDARA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI

  1. Kutunga na kusimamia, kutathmini na kupitia utekelezaji wa sera za maendeleo ya utamaduni sheria,kanuni na miongozo mbali mbali.
  2. Kusimamia na kuratibu utendaji kazi wa taasisi za kiutamaduni zilizo chini ya wizara.
  3. Kuanzisha na kuibua programu za ushirikiano na ubadilishanaji wa maarifa,uzoefu na ujuzi wa kiutaduni baina ya Tanzania na Mtaifa mengine.
  4. Kutoa tuzo kwa kazi za utamaduni kupitia matukio ya kiutamaduni.
  5. Kutoa miongozo mbalimbali kuhusiana na misingi ya maadili ya Taifa.
  6. Kukuza,kuwezesha na kuratibu ujenzi wa uwezo wa rasilimali watu ya kiutamaduni kwa kushirikiana na waajiri wa karibu.
  7. Kuanzisha mbinu za kuendeleza, kutangaza masuala ya mila, desturi na lugha;
  8. Kutoa ushauri juu ya masuala yanayohusiana na maadili katika kuandaa sinema, filamu/uigizaji, maonesho na utoaji wa leseni katika maeneo hayo.
  9. Kuratibu na kushiriki matukio, semina, warsha, makongamano na mafunzo mbalimbali yanayohusu utamaduni na lugha.
  10. Kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa watendaji wa kazi za utamaduni.

Idara ya Maendeleo ya Utamaduni ina sehemu kuu mbili.

  • Sehemu ya urithi wa utamaduni na maadili ya Taifa.
  • Sehemu ya Lugha.

1. Majukumu ya sehemu ya urithi wa utamaduni na maadili ya Taifa.

  • Kuendeleza, kutafuta, kutathmini na kupitia upya utekelezaji wa sera na sheria za utamaduni za kitaifa.
  • Kuunda, kuendeleza na kutekeleza mikakati na miongozo kwaajili ya kukuza ubunifu wa utamaduni wa jadi na kitaifa na kufanya kazi na kuisambaza.
  • Kutetea utekelezaji wa sera ya utamaduni wa kitaifa kwa ajili ya kukuza utamaduni na utambulisho wa Taifa.
  • Kuandaa na kutoa miongozo ya ujumuishaji wa kanuni na maadili ya kitamaduni katika mipango ya maendeleo ya kijamii,kiuchumi na kisiasa na kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.
  • Kusoma na kuamua mila mbalimbali zinazokuza na kuathiri maendeleo ya utamaduni wa Taifa.
  • Kuendeleza mifumo ya kukuza programu za kubadilishana utamaduni wa kimataifa.
  • Kufanya utafiti na kuandaa orodha ya mila na desturi zinazokubalika na zisizokubalika zinazoathiri maendeleo ya Taifa.
  • Kuandaa miongozo ya uundaji na usimamizi wa vikundi vya kitamaduni nchini na kufuatilia na kutathmini utekelezaji.
  • Kuhifadhi utafiti, kumbukumbu na kukuza historia ya mapambano ya ukombozi wa mwafrika nchini Tanzania.
  • Kuratibu shughuli za utafiti wa mila na desturi.
  • Kuandaa na kuratibu matukio ya Tamasha za kiutamaduini zinazofanyika nchini.
  • Kuhamasisha wadau kuanzisha miundombinu ikiwa ni pamoja na Makumbusho, Kituo cha utamaduni, kumbi za kudumu za maonyesho ya utamaduni na warsha za ufundi na bidhaa asilia.
  • Kushauri juu ya tathmini ya athari za kiutamaduni zinazohusiana na miradi ya maendeleo.
  • Kuendesha na kuratibu kampeni ya elimu ya juu ya maadili.

2. Majukumu ya sehemu ya lugha.

  • Kuendeleza, kufuatilia, kutathmini na kupitia upya utekelezaji wa sera ya utamaduni wa kitaifa (Lugha).
  • Kuendeleza na kutekeleza mikakati na taratibu za kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika utawala wa serikali, elimu, siasa, jumuiya ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani.
  • Kuandaa na kusambaza sheria na miongozo ya utekelezaji wa sera ya utamaduni (Lugha).
  • Kutetea utekelezaji wa sera ya utamaduni ili kukuza lugha ya Kiswahili kwa ajili ya kukuza Sanaa za jadi na zisizo za jadi.
  • Kuwezesha,Kufuatilia na kutathmini utendaji kazi wa BAKITA na Kamisheni ya Kiswahili ya Afika Mashariki
  • Kuandaa na kutoa miongozo mbalimbali juu ya uanzilishaji na uendeshaji wa vyama vya lugha na fasihi pamoja na kusimamia utekelezaji wake.
  • Kuandesha na kuratibu semina na warsha kwa vyombo vya habari kuhusiana na matumizi fasaha ya lugha ya Kiswahili.
  • Kuandaa na kuratibu mipango mikakati ya kuendesha tafiti, uchapishaji na utunzaji wa nyaraka mbalilmbali kuhusiana na lugha za makabila kwa ajili ya kukuza istilahi na msamiati wa lugha ya Kiswahili.
  • Kuhamasisha na kuratibu uanzishaji wa vituo vya kufundisha lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi (kwenye Balozi za Tanzania).
Idara ya Maendeleo ya Sanaa

Idara ya Maendeleo ya Sanaa imeundwa baada ya muundo mpya wa Wizara. Kabla ya hapo Idara ilikuwa ni sehemu ndani ya Idara ya Maendeleo ya Utamaduni. Kwa mwaka wa fedha 2016/2017 idara ilitekeleza majukumu yake ikiwa pamoja na Idara ya Maendeleo ya Utamaduni.

Idara ya Sanaa ndiyo yenye dhamana ya kusimamia maendeleo ya Sekta ya Sanaa nchini. Sanaa hizo ni pamoja na filamu, muziki, michezo ya kuigiza, ngoma, dansi, sarakasi na kazi za mikono kama vile uchoraji, uchongaji, uhunzi, usukaji, ufumaji, ushonaji na ususi.

Idara ya Sanaa inajukumu la kusimamia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) na Bodi ya Filamu Tanzania.

Idara ya Maendeleo ya Sanaa imegawanyika katika kuu sehemu mbili;-

2. Sehemu ya haki na Maendeleo ya wasanii (Sehemu hizi zitaongozwa na Wakurugenzi wasaidizi wawili 2)

MAJUKUMU YA IDARA YA MAENDELEO YA SANAA

Majukumu ya Idara ya Maendeleo ya Sanaa ni haya yafuatayo;-

I.Kusimamia na kuratibu uandaaji wa Sera ya Maendeleo ya Sanaa.

II.Kuandaana kutoa miongozo ya kusimamia utekelezaji wa shughuli za Sanaa na Ubunifu.

III.Kuendeleza, kufuatilia, kutathmini na kurekebisha utekelezaji waSheria na Miongozo ya Sera ya Sanaa,


  1. MAJUKUMU YA SEHEMU YA URATIBU WA TASNIA YA SANAA

Majukumu ya Sehemu ya Uratibu wa Tasnia ya Sanaa ni:-

i.Kuendeleza, Kuratibu na kutekeleza mbinu za kiutendaji za shughuli za sanaa .

ii.Kuendeleza, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera ya kitaifa ya sanaa, sheria na miongozo katika muziki, sanaa za maonesho na ubunifu kwa ujumla.

iii.Kudhibiti na kusisitiza matumizi ya maadili ya kitaifa katika shughuli za muziki, sanaa za maonesho na ubunifu kwa jumla .

iv.Kuratibu na kuendeleza mifumo ya kutambua na kutoa tuzo kwa wasanii na taasisi bora katika kutekeleza shughuli za maendeleo ya sanaa.

v.Kuratibu na kusimamia taasisi za sanaa za Tanzania, wanamuziki, sanaa za maonyesho, na wataalamu wa sanaa wanaofanya vizuri katika Tasnia.

vi.Kufuatilia na kutathmini majukumu nakazi ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuba), bodi ya Ukaguzi wa filamu na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

vii.Kuratibu na kusimamia nakutoa miongozo yautekelezaji wa Sera ya Taifa ya filamu. MAJUKUMU YA SEHEMU YA HAKI NA MAENDELEO YA WASANII.

Majukumu ya Sehemu ya haki na Maendeleo ya Wasanii ni:-

i.Kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa Programu mbalimbali za wasanii.

ii.Kuratibu na kusimamia mikataba ya wasanii na kazi zao

iii.Kuratibu na kutoa ujuzi wa ujasiriamali na kitaaluma.

iv.Kuratibu, kubuni na kutekeleza miradi ili kukuza wasanii na kazi zao.

v.Kuratibu makundi ya sanaa, vyama na mashirikisho.

vi.Kuratibu, kusimamia, kudhibiti na kutoa miongozo ya ulinzi wa kazi za wasanii ikiwa ni pamoja na haki miliki.

vii. Kuratibu na kufuatilia haki za wasanii kwa kushirikiana na taasisi inayohusikana hakimiliki na hakishiriki.

Idara ya Maendeleo ya Michezo

To provide expertIDARA YA MAENDELEO YA MICHEZO

1.Utangulizi

Sekta ya Michezo hapa nchini imekuwa ikisimamiwa na Sera ya Maendelo ya Michezo yam waka 1995. Malengo ya Sera hiyo ni pamoja na kuhamasisha Umma wa Watanzania kushiriki katika Michezo na mazoezi ya viungo; kuwezesha upatikanajio wa Viwanja na zana bora na za kutosha kwa ajili ya kuimarisha Maendeleo ya Michezo nchini, kuandaa na kutayarisha wataalamu wa kutosha katika fani na taaluma mbali mbali za Michezo ya Kimataifa. Malengo mengine ni kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika utoaji wa Elimu kwa Michezo na kuimarisha utafiti katika Michezo ya jadi kwa lengo la kuiendeleza. Idara ya Maendeleo ya Michezo ndipyo chombo cha juu cha Wizara ambacho kinasimamia utekelezaji wa Sera hiyo hapa nchini Tanzania.

2.Majukumu ya Idara ya Maendeleo ya Michezo.

Katika kuhakisha Tanzania inanufaika na Sekta ya Michezo, Serikali ilitunga Sera ya Maendeleo ya Michezo yam waka 1995 ambayo ilibainisha malengo mbali mbali ya kutekelezwa kupitia mgawanyo wa majukumu yaliyobainishwa na Sera hiyo kama ifuatavyo:

(i)Uhamasishaji kwa Umma wa Tanzania kushiriki katika Michezo na mazoezi ya viungo vya mwili

(ii)Upatikanaji wa viwanja vya kutosha kwa ajili ya kuimarisha maendeleo ya Michezo

(iii)Upatikanaji wa zana bora za Michezo ili kuimarisha Michezo

(iv)Uuandaaji na utayarishaji kwa Wataalamu wa kutosha katika fani na taaluma mbali mbali za Michezo

(v)Kuhakikisha Timu na wachezaji wanafanya vizuri katika Michezo na Mashindano ya Kimataifa

(vi)Utafiti katika Michezo ya Jadi kwa lengo la kuifufua na kuindeleza.

(vii)Ushirikiano na Mataifa mengine katika utoaji wa Elimu kwa Michezo na Michezo

(viii)Mgawanyo wa Majukumu katika utekelezaji wa Sera

3.Muundo wa Idara ya Maendeleo ya Michezo

Idara ya Maendeleo ya Michezo imegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni sehemu ya maendeleo ya Michezo na sehemu inayoshughulikis maendeleo ya miundo mbinu ya Michezo. Kwa mujibu wa Muundo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Micheo. Idara ya Maendeleo ya Michezo ina Taasisi mbili ambazo zinafanya kazi na Idara. Taasisi hizo ni; chuo cha Maendeleo ya Michezo Mlya na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

i.Baraza la Michezo la taifa ni Taasisi iliyoundwa kwa ksheria ya Bunge ya Na.12 ya mwaka 1967. Kwa mujibu wa sheria hiyo Baraza lina majukumu yafuatayo

ii.Kuvisaidia na kuviendeleza vyama vya Michezo kwa kuandaa mafunzo kwa viongozi wa vyama na vilabu vya Michezo

iii. Kutoa ushauri kwa vyama vya Michezo juu ya ujenzi wa viwanja vya Michezo

iv.Kutafuta vifaa vya Michezo na kuvisambaza kwa wanaohitaji

v.Kuandaa utaratibu wa kujenga uhusianio wa kimichezo kati ya Vyama vya Michezo na Wachezaji wenyewe

vi.Kuchambua na kuthibitisha ratiba za masshindano ya Michezo zinazoandaliwa na vyama vya Michezo

vii.Kuandaa Tamasha la Michezo kitaifa kwa kushirikiana na vyama vya Michezo

viii.Kuishauri Wizara juu ya uhusiano wa kimichezo na Mataifa mengine

ix.Kuandaa na kutekelez mbinu mbali mbali za kusisimua mwamko wa Michezo kwa ujumla, kama vile kutenegeza na kutoa medali za Michezo, kutoa misaada au nafasi za mafunzo ya Michezo (Scholarship), kuendesha zahanati za Michezo

x.Kuhakikisha kuwa fedha za vyama vya Michezo zinakaguliwa na matumizi mabaya ya fedha yanaondolewa katika vyama hivyo.ise and services in policy formulation, implementation, monitoring and evaluation

Administration and Human Resource Management Division

Objectives

To provide expertise and services on human resources management and administrative matters to the Ministry.

Functions

To provide strategic inputs to management on Administration and Human resources Management issues

To provide link between the Ministry and the President’s Office Public Service Management on operationalization of the Public Service Management and Employment Policy of 1998 and Public Service Act No. 8 of 2002

The Division is led by the Director and comprise two Sections as follows;

Administration Section

Human Resources Management Section

Idara ya Sera na Mipango

UTANGULIZI

Idara ya Sera na Mipango inatekeleza majukumu yake kupitia Sehemu ya Sera, Sehemu ya Mipango na Bajeti na Sehemu ya Ufuatiliaji na Tathimini.

MAJUKUMU YA IDARA YA SERA NA MIPANGO

Kazi kuu ya Idara hii ni kuratibu shughuli zote zinazotekelezwa na Wizara. Aidha, Idara hii hutoa utaalamu na huduma kwa masuala ya utungaji, utekelezaji, kufuatilia na kutathmini Sera za Wizara. Vilevile, Idara hii ni kiunganishi kati ya Idara na Vitengo vyote Wizarani. Majukumu mengine ni pamoja na:

  1. Kuratibu utungaji wa Sera za Wizara, kufuatilia utekelezaji wake na kufanya tathimini;
  2. Kuchambua nyaraka mbalimbali kutoka Asasi nyingine na kushauri juu ya nyaraka hizo;
  3. Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa Mipango na Bajeti ya Wizara;
  4. Kufanya Ufuatiliaji na Tathimini ya Mipango na Bajeti na kuandaa taarifa ya utekelezaji;
  5. Kufanya utafiti, tathimini ya mipango ya Wizara na kutoa uamuzi wa mwelekeo wa mbele wa Wizara;
  6. Kumotisha na kuwezesha utoaji wa huduma kwa Wizara kwa kutumia sekta binafsi;
  7. Kuratibu maandalizi ya michango ya Hotuba za Bajeti na Taarifa za Uchumi za mwaka za Wizara;
  8. Kujenga uwezo wa Mpango Mkakati, Bajeti, Ufuatiliaji na Tathimini katika Wizara; na
  9. Kuhakikisha kuwa Mipango na Bajeti za Wizara inajumuishwa katika Mipango na Bajeti za Serikali

UONGOZI NA UTAWALA

Idara ya Sera na Mipango inaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango na kusaidiwa na Wakurugenzi Wasaidizi kwa kila sehemu.

Procurement and Supply

FUNCTIONS OF PROCUREMENT MANAGEMENT UNIT

Objective

To provide expertise and services in procurement, storage and supply of goods and services for the Ministry This Unit will perform the following activities: -

  1. Develop an Annual Procurement Plan for the Ministry
  2. Advise the Management on matters pertaining to procurement of goods, services and logistics management
  3. Monitor adherence to procurement process and procedures as per Public Procurement Act
  4. Procure, maintain and manage supplies, materials and services to support the logistics requirement of the Ministry
  5. Maintain and monitor distribution of office supplies and materials
  6. Provide Secretariat to the Tender Board as per Public Procurement Act; and
  7. Set specifications/standards for goods and services procured and monitor