Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Kuundwa kwa Wizara

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iliundwa na Serikali tarehe 08 Desemba, 2024 na kuchapishwa katika Tangazo la Serikali Na. 36 la tarehe 17 Januari, 2025. Wizara imekabidhiwa majukumu ya kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria na Mipango mbalimbali ya Serikali katika Sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Vilevile, Wizara ina jukumu la kusimamia shughuli za maendeleo ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini.

Wizara kimuundo imegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni:

  1. Usimamizi na utekelezaji wa masuala ya kisekta
  2. Uendeshaji, uratibu na usimamizi

USIMAMIZI NA UTEKELEZAJI WA MASUALA YA KISEKTA

Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Habari, Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, Idara ya Maendeleo ya Sanaa na Idara ya Maendeleo ya Michezo kwa ushirikiano na Taasisi zilizopo chini ya Idara hizo.

UENDESHAJI URATIBU NA USIMAMIZI

  • Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Sera na Mipango, Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Kitengo cha Fedha na Uhasibu, Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Kitengo cha Huduma za Sheria, Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini pamoja na Kitengo cha Tathmina na Ufuatiliaji.
  • Kuendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji mzuri wa Habari, Kukuza Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Maendeleo ya Jamii na Uchumi.