Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Habari

SINGELI MBIONI KUTAMBULIKA KAMA URITHI WA TAIFA UNESCO


Katibu Mkuu wa  Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndg Gerson Msigwa amesema tayari wameshaanza kupeleka Maandiko Katika Shirika Elimu  Sayansi na  Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO)  kwa ajili ya Kuutambulisha Mziki wa Singeli kama urithi wa Taifa kwa kuwa ni  Muziki wenye vionjo na radha za kwetu.

Msigwa amesema hayo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari  kuelekea uzinduzi wa  mashindano ya CHAN 2024, yanayotarajiwa kuzinduliwa Agosti 02, 2025 katika Uwanja wa Benjamini Mkapa.

Msigwa amesema katika mashindano hayo, mbali na Soka kutakuwa na Tamasha kubwa la muziki wa singeli  ambapo pamoja na mambo mengine wanahamasisha kwa kiasi kikubwa muziki huo kwa kuwa umeshika kasi duniani kote hivyo wanataka Dunia Itambue muziki huo  asili yake ni Tanzania.

Pia ametoa onyo wa wale ambapo wanatumia sanaa hiyo kuimba   hovyo kwani watawashughulikia ili  kunusuru Kazi hiyo na kuwataka vijana kuona fursa ya ajira na kuutumia vizuri kwani unalipa.

Kutokana na hayo  Wizara imefunga Jukwaa kubwa katika Uwanja wa Taifa ambapo mara ya baada ya mechi ya ufunguzi, Agosti 02, 2025 kati ya  Tanzania na Burkina Faso Kumalizika, watu wataendelea kuburudika na muziki huo wa Singeli na hivyo kuwakataka wananchi wajitokeze kwa wingi wakaburudike  na Burudani mbalimbali.