Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa ameongoza Watumishi wa Wizara hiyo, katika zoezi la upandaji miti ikiwa ni mwendelezo wa kutekeleza azma ya Serikali ya upandaji miti ili kuhifadhi mazingira. Zoezi hilo limefanyika leo Februari 06, 2026 katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma.