Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amesema Serikali itaendelea kuboresha viwanja mbalimbali nchini ili viweze kutumika katika michuano ya kimataifa hata baada ya Mashindano ya kombe la Mataifa Afrika mwaka 2027(AFCON 2027). Kauli hiyo ameitoa Juni 03, 2026 jijini Tanga mara baada ya kutembelea na kukagua usimikaji wa viti katika Uwanja wa CCM Mkwakwani.