Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Habari

WAZIRI MAKONDA AAHIDI  MILIONI 20 KWA AFISA MICHEZO ATAKAYEFANYA VIZURI


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.  Paul Makonda ameahidi zawadi ya shilingi Milioni 20 kwa Afisa  Maendeleo ya Michezo ambaye atafanikiwa kuwa na michezo 20 inayofanya vizuri kwenye Wilaya yake.

Makonda amesema hayo leo Machi  28, 2026   wakati akifungua  Kikao kazi cha 16 cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo, kwenye Ukumbi wa  AICC Jijini Arusha, huku akisisitiza kuwa, hatua  hiyo inalenga  kufufua vipaji vya  vijana na kuwawezesha kiuchumi na kuitangaza nchi Kimataifa.

"Ninawaelekeza kwamba,  mwakani tutakapokutana kila mmoja kwenye Wilaya yake awe na michezo angalau 20, atakayefanya vizuri tutampa zawadi na ataenda nayo nyumbani kwake", zawadi hiyo itakabidhiwa kwenye kikao cha 17 pamoja na Wizara   kumtambua mshindi huyo alisema Makonda"