Habari
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI KIWANDA CHA UCHAPAJI (TSN)
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imeoneshwa kurudhishwa na mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha uchapaji inaoendelea katika Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) ambao umefikia Asilimia 71.
Kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Mhe. Husna Sekiboko wakati wa ziara hiyo katika kampuni hiyo wamepokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda ambaye ameeleza kuwa mradi huo unalenga kupanua uzalishaji wa biashara ya uchapishaji, na kuwezesha kampuni kujitegemea na kutoa gawio kwa Serikali.
Kiwanda hicho ambacho kitakuwa na mashine 18 ambapo kwa sasa zimeshafungwa kwa asilimia 85 kinatarajiwa kuwa na uwezo mkubwa zaidi na kufanya vyema katika ushindani wa biashara ya Uchapaji Sokoni.
