Habari
SERIKALI YASISITIZA UJENZI WA ARENA KUBWA YA KISASA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ina mpango wa kujenga arena kubwa ya kisasa itakayokuwa kitovu cha matukio mbalimbali ya michezo na burudani nchini.
Akizungumza usiku wa kuamkia Julai 31 2026 wakati tamasha la mchezo wa Masumbwi “Knockout ya Mama Season 9” liliofanyika katika ukumbi wa The super Dome Masaki jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Nchemba amesema, Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kukuza vipaji vya vijana kupitia uwekezaji katika sekta ya michezo na ujenzi wa miundombinu ya kisasa.
Amesitiza kuunga mkono juhudi za vijana na wadau wa michezo nchini, huku Serikali ikiendelea kushirikiana kwa karibu na sekta binafsi katika kuimarisha maendeleo ya michezo na kuibua vipaji.
