Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

Habari

MWINJUMA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA UGANDA KUJADILI MAANDALIZI YA AFCON


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, ameongoza Ujumbe maalumu wa Kamati ya maandalizi ya AFCON 2027 kutoka Tanzania ambao umewasili nchini Uganda, jana Aprili 21, 2026.
 
Ujumbe huo unatarajiwa kushiriki katika mkutano  unaowakutanisha wajumbe wa kamati tatu za maandalizi za nchi wenyeji yani Tanzania,  Kenya na Uganda ikiwa ni miongoni mwa juhudi za pamoja za kuhakikisha maandalizi ya AFCON 2027, yatakayofanyika kuanzia Juni 19 hadi Julai 18, 2027, yanaenda kwa kasi na kwa ubora unaokidhi viwango vya Shirikisho la Soka Afrika (CAF).