Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla akiongozana Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, wakati akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), linapofanyika Kongamano la Tano la Idhaa za Kiswahili Duniani, leo Machi 24, 2026.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, akiiaga na kuikabidhi bendera ya Taifa timu ya mpira wa kikapu ya Dar City ikiwa ni ishara ya kuwatakia mafanikio katika ligi ya mchezo wa kikapu Afrika (Basketball Africa League) (BAL) inayotarajiwa kuanza Machi 27, 2026 Pretoria Afrika Kusini.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Christian Makonda, ameshiriki na kufanikiwa kumaliza mbio za kilomita 5 katika Kilimanjaro International Marathon 2026 iliyofanyika Moshi. Ushiriki wake unaonyesha kuunga mkono jitihada za kukuza michezo, afya na ustawi wa jamii kupitia matukio ya kimataifa.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Christian Makonda, ameshiriki na kufanikiwa kumaliza mbio za kilomita 5 katika Kilimanjaro International Marathon 2026 iliyofanyika Moshi. Ushiriki wake unaonyesha kuunga mkono jitihada za kukuza michezo, afya na ustawi wa jamii kupitia matukio ya kimataifa.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Christian Makonda, ameshiriki na kufanikiwa kumaliza mbio za kilomita 5 katika Kilimanjaro International Marathon 2026 iliyofanyika Moshi. Ushiriki wake unaonyesha kuunga mkono jitihada za kukuza michezo, afya na ustawi wa jamii kupitia matukio ya kimataifa.
Picha ya Uwanja wa Arusha ambao kwa sasa umefikia 74%. Uwanja huu unatarajiwa kutumika katika Mashindano ya AFCON 2027 na unatarajiwa kukamilika Julai mwaka huu (2026).
Viongozi na watumishi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakiongozwa na Waziri, Mhe. Paul Makonda, leo Januari 14, 2026, wamepanda miti mbalimbali ikiwemo ya matunda na kivuli kwenye jengo la Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma,
Makabidhiano ya Ofisi ya aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi na Waziri mpya Mhe. Paul Makonda
Wataalamu wa Sekta ya Michezo katika Umoja wa Afrika Kanda ya 4, wakiwa katika siku ya pili ya mkutano wa pili wa kanda hiyo ngazi ya wataalamu, wenye lengo la kujadili maendeleo ya michezo katika ukanda huo leo Agosti 19, 2025, jijini Dar es Salaam.